Skip to content
Mithali 4:10-19

Mithali 4:10-19

10
Sikiliza mwanangu, kubali ninachokuambia, nayo miaka ya maisha yako itakuwa mingi.
11
Ninakuongoza katika njia ya hekima na kukuongoza katika mapito yaliyonyooka.
12
Utembeapo, hatua zako hazitazuiliwa; ukimbiapo, hutajikwaa.
13
Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako.
14
Usiuweke mguu wako katika njia ya waovu wala usitembee katika njia ya watu wabaya.
15
Epukana nayo, usisafiri katika njia hiyo; achana nayo, na uelekee njia yako.
16
Kwa kuwa hawawezi kulala mpaka watende uovu; wanashindwa hata kusinzia mpaka wamwangushe mtu.
17
Wanakula mkate wa uovu, na kunywa mvinyo wa jeuri.
18
Njia ya wenye haki ni kama nuru ya kwanza ya mapambazuko, ambayo hungʼaa zaidi na zaidi mpaka mchana mkamilifu.
19
Lakini njia ya waovu ni kama giza nene; hawajui kinachowafanya wajikwae.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options