Mithali 4:1-9
1
Sikilizeni wanangu, mafundisho ya baba yenu; sikilizeni kwa makini na mpate ufahamu.
2
Ninawapa mafundisho ya maana, kwa hiyo msiyaache mafundisho yangu.
3
Nilipokuwa mvulana mdogo katika nyumba ya baba yangu, ningali mchanga na mtoto pekee kwa mama yangu,
4
baba alinifundisha akisema, “Yashike maneno yangu yote kwa moyo wako wote; yashike maagizo yangu na wewe utaishi.
5
Pata hekima, pata ufahamu; usiyasahau maneno yangu wala usiyaache.
6
Usimwache hekima naye atakuweka salama; mpende, naye atakulinda.
7
Hekima ni bora kuliko vitu vyote; kwa hiyo jipe hekima. Hata ikikugharimu vyote ulivyo navyo, pata ufahamu.
8
Mstahi, naye atakukweza; mkumbatie, naye atakuheshimu.
9
Atakuvika shada la neema kichwani mwako na kukupa taji ya utukufu.”
Settings