Mithali 3:21-26
21
Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
22
ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
23
Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
24
ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
25
Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
26
kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
Settings