Mithali 3:13-20
13
Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
14
kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
15
Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
16
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
17
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
18
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
19
Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
20
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
Settings