Skip to content
Mithali 24:23-29

Mithali 24:23-29

23
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options