Mithali 23:9
Inaonyesha mstari 9 pamoja na muktadha unaouzunguka.
6
Usile chakula cha mtu mchoyo, usitamani vyakula vyake vitamu,
7
kwa maana yeye ni aina ya mtu ambaye kila mara anafikiri juu ya gharama. Anakuambia, “Kula na kunywa,” lakini moyo wake hauko pamoja nawe.
8
Utatapika kile kidogo ulichokula, nawe utakuwa umepoteza bure maneno yako ya kumsifu.
9
Usizungumze na mpumbavu, kwa maana atadhihaki hekima ya maneno yako.
10
Usisogeze jiwe la mpaka wa zamani wala kunyemelea kwenye mashamba ya yatima,
11
kwa kuwa Mtetezi wao ni mwenye nguvu, atalichukua shauri lao dhidi yako.
12
Elekeza moyo wako kwenye mafundisho na masikio yako kwenye maneno ya maarifa.
Settings