Rukia maudhui
Mithali 22:17-21

Utangulizi wa Maneno ya Wenye Hekima

Mithali 22:17-21
17
Tega sikio na usikie misemo ya wenye hekima, elekeza moyo wako kwenye yale nifundishayo,
18
kwa maana inapendeza unapoyahifadhi moyoni mwako na kuwa nayo yote tayari midomoni mwako.
19
Ili tumaini lako liwe katika Bwana, hata wewe, ninakufundisha leo.
20
Je, sijakuandikia misemo thelathini, misemo ya mashauri na maarifa,
21
kukufundisha maneno ya kweli na ya kuaminika, ili uweze kutoa majibu sahihi kwake yeye aliyekutuma?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options