Mithali 21:20-26
20
Katika nyumba ya mwenye hekima kuna akiba ya vyakula vizuri na mafuta, lakini mtu mpumbavu hutafuna vyote alivyo navyo.
21
Yeye afuatiaye haki na upendo hupata uzima, mafanikio na heshima.
22
Mtu mwenye hekima huushambulia mji wa wenye nguvu, na kuangusha ngome wanazozitegemea.
23
Yeye alindaye kinywa chake na ulimi wake hujilinda na maafa.
24
Mtu mwenye kiburi na majivuno, “Mdhihaki” ndilo jina lake; hutenda mambo kwa kiburi kilichozidi.
25
Kutamani sana kwa mvivu kutakuwa kifo chake, kwa sababu mikono yake haitaki kufanya kazi.
26
Mchana kutwa hutamani zaidi, lakini mnyofu hutoa pasipo kuzuia.
Settings