Mithali 21:27-31
27
Dhabihu ya mtu mwovu ni chukizo, si zaidi sana itolewapo kwa nia mbaya!
28
Shahidi wa uongo ataangamia, bali maneno ya mwenye kusikia yatadumu.
29
Mtu mwovu ana uso wa ushupavu, bali mtu mnyofu huzifikiria njia zake.
30
Hakuna hekima, wala akili, wala mpango unaoweza kufaulu dhidi ya Bwana.
31
Farasi huandaliwa kwa ajili ya siku ya vita, bali ushindi huwa kwa Bwana.
Settings