Skip to content
Mithali 21:10-19

Mithali 21:10-19

10
Mtu mwovu hutamani sana ubaya, jirani yake hapati huruma kutoka kwake.
11
Wakati mwenye mzaha ameadhibiwa, mjinga hupata hekima; wakati mtu mwenye hekima afundishwapo, hupata maarifa.
12
Mwenye Haki huyajua yanayotendeka katika nyumba za waovu, naye atawaangamiza waovu.
13
Mtu akiziba masikio asisikie kilio cha maskini, yeye pia atalia, wala hatajibiwa.
14
Zawadi itolewayo kwa siri hutuliza hasira na rushwa iliyofichwa kwenye nguo hutuliza ghadhabu kali.
15
Wakati haki imetendeka, huleta furaha kwa wenye haki, bali kitisho kwa watenda mabaya.
16
Mtu anayepotea kutoka mapito ya ufahamu, hupumzika katika kundi la waliokufa.
17
Mtu apendaye anasa atakuwa maskini, yeyote apendaye mvinyo na mafuta kamwe hatakuwa tajiri.
18
Waovu huwa fidia kwa ajili ya wenye haki, nao wasio waaminifu kwa ajili ya wanyofu.
19
Ni afadhali kuishi jangwani kuliko kuishi na mke mgomvi na mkorofi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options