Mithali 16:8-12
8
Afadhali kitu kidogo pamoja na haki kuliko mapato mengi pamoja na udhalimu.
9
Moyo wa mtu huifikiri njia yake, bali Bwana huelekeza hatua zake.
10
Midomo ya mfalme huzungumza kwa hekima ya kiungu, wala kinywa chake hakipotoshi haki.
11
Vipimo na mizani za halali hutoka kwa Bwana; mawe yote ya kupimia yaliyo katika mfuko ameyafanya yeye.
12
Wafalme huchukia sana kutenda maovu, kwa maana kiti cha ufalme hufanywa imara kwa njia ya haki.
Settings