Hesabu 13:3-16
3
Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli.
4
Haya ndiyo majina yao: kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;
5
kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;
6
kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;
7
kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;
8
kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;
9
kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;
10
kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,
11
kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;
12
kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;
13
kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;
14
kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;
15
kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.
16
Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)
Settings