Skip to content
Hesabu 10:14-27

Hesabu 10:14-27

14
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
15
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
16
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
17
Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
18
Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
19
Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
20
naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
21
Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
22
Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
23
Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
24
naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
25
Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
26
Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
27
naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options