Mathayo 26:6-9
6
Yesu alikuwa Bethania nyumbani mwa Simoni aliyekuwa na ukoma,
7
naye mwanamke mmoja akamjia akiwa na chupa ya marhamu yenye manukato ya thamani kubwa; akayamimina kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani kula chakula.
8
Lakini wanafunzi wake walipoona hayo wakakasirika, wakasema, “Upotevu huu wote ni wa nini?
9
Manukato haya yangeuzwa kwa bei kubwa, na fedha hizo wakapewa maskini.”
Settings