Mathayo 24:15-22
15
“Hivyo mtakapoona lile ‘chukizo la uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu),
16
basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani.
17
Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke ili kuchukua chochote kutoka ndani ya nyumba.
18
Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.
19
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!
20
Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya Sabato.
21
Kwa maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa: wala haitakuwako tena kamwe.
22
Kama siku hizo zisingefupishwa, hakuna hata mtu mmoja ambaye angeokoka. Lakini kwa ajili ya wateule, siku hizo zitafupizwa.
Settings