跳到主要内容
Mathayo 24:15-21

Mathayo 24:15-21

15
“Hivyo mtakapoona lile ‘chukizo la uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli limesimama mahali patakatifu (asomaye na afahamu),
16
basi wale walioko Uyahudi wakimbilie milimani.
17
Yeyote aliye juu ya dari ya nyumba asishuke ili kuchukua chochote kutoka ndani ya nyumba.
18
Aliye shambani asirudi nyumbani kuchukua vazi lake.
19
Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!
20
Ombeni ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya Sabato.
21
Kwa maana wakati huo kutakuwa na dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu mwanzo wa dunia mpaka sasa: wala haitakuwako tena kamwe.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options