Skip to content
Mathayo 10:26-31

Mathayo 10:26-31

26
“Kwa hiyo msiwaogope hao, kwa maana hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna siri ambayo haitajulikana.
27
Ninalowaambia gizani, ninyi lisemeni mchana peupe. Na lile mnalosikia likinongʼonwa masikioni mwenu, lihubirini juu ya nyumba.
28
Msiwaogope wale wauao mwili lakini hawawezi kuua roho. Afadhali mwogopeni yeye awezaye kuiangamiza roho na mwili katika jehanamu.
29
Je, shomoro wawili hawauzwi kwa senti moja tu? Lakini hakuna hata mmoja wao atakayeanguka chini pasipo Baba yenu kujua.
30
Hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa.
31
Hivyo msiogope; kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options