Marko 3:14-19
14
Akawachagua kumi na wawili, ambao aliwaita mitume, ili wapate kuwa pamoja naye, na awatume kwenda kuhubiri
15
na kuwa na mamlaka ya kutoa pepo wachafu.
16
Hawa ndio wale kumi na wawili aliowachagua: Simoni (ambaye alimwita Petro);
17
Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye (ambao aliwaita Boanerge, maana yake Wana wa Ngurumo);
18
Andrea, Filipo, Bartholomayo, Mathayo, Tomaso, Yakobo mwana wa Alfayo, Thadayo, Simoni Mkananayo,
19
na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
Settings