Luka 23:20-25
20
Pilato, akitaka kumwachia Yesu, akasema nao tena.
21
Lakini wao wakaendelea kupiga kelele wakisema, “Msulubishe! Msulubishe!”
22
Kwa mara ya tatu, Pilato akawauliza, “Kwani amefanya kosa gani huyu mtu? Sikuona kwake sababu yoyote inayostahili adhabu ya kifo. Kwa hiyo nitaamuru apigwe mijeledi, na kisha nitamwachia.”
23
Lakini watu wakazidi kupiga kelele kwa nguvu zaidi, wakidai kwamba Yesu asulubiwe. Hivyo, kelele zao zikashinda.
24
Kwa hiyo Pilato akatoa hukumu kwamba madai yao yatimizwe.
25
Akamfungua yule mtu aliyekuwa amefungwa gerezani kwa kuhusika katika uasi dhidi ya serikali na mauaji. Akamkabidhi Yesu mikononi mwao, wamfanyie watakavyo.
Settings