Skip to content
Yohana 4:3

Yohana 4:3

Inaonyesha mstari 3 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Mafarisayo wakasikia kwamba Yesu alikuwa anapata na kubatiza wanafunzi wengi zaidi kuliko Yohana,
2
ingawa kwa kweli si Yesu mwenyewe aliyekuwa akibatiza, ila ni wanafunzi wake.
3
Bwana alipojua mambo haya, aliondoka Uyahudi akarudi tena Galilaya.
4
Wakati huo ilimlazimu apitie Samaria.
5
Akafika kwenye mji mmoja wa Samaria uitwao Sikari, karibu na lile shamba ambalo Yakobo alimpa mwanawe Yosefu.
6
Huko ndiko kulikokuwa na kile kisima cha Yakobo. Naye Yesu alikuwa amechoka kwa kuwa alikuwa ametoka safarini. Akaketi karibu na hicho kisima. Ilikuwa yapata saa sita mchana.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 90 chars

Options