Skip to content
Yohana 14:1-6

Yohana 14:1-6

1
Yesu akawaambia, “Msifadhaike mioyoni mwenu, mnamwamini Mungu, niaminini na mimi pia.
2
Nyumbani kwa Baba yangu kuna makao mengi. Kama sivyo, ningeliwaambia. Naenda kuwaandalia makao.
3
Nami nikienda na kuwaandalia makao, nitarudi tena na kuwachukua mkae pamoja nami, ili mahali nilipo, nanyi mpate kuwepo.
4
Ninyi mnajua njia ya kufika ninakokwenda.”
5
Tomaso akamwambia, “Bwana, sisi hatujui unakokwenda, tutaijuaje njia?”
6
Yesu akawaambia, “Mimi ndimi njia na kweli na uzima. Mtu hawezi kuja kwa Baba isipokuwa kwa kupitia kwangu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options