Yohana 12:37-43
37
Hata baada ya Yesu kufanya miujiza hii yote mbele yao, bado hawakumwamini.
38
Hili lilikuwa ili kutimiza lile neno la nabii Isaya lililosema: “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu, na mkono wa Bwana umefunuliwa kwa nani?”
39
Kwa hivyo hawakuamini, kwa sababu Isaya anasema mahali pengine:
40
“Amewafanya vipofu, na kuifanya mioyo yao kuwa migumu, ili wasiweze kuona kwa macho yao, wala kuelewa kwa mioyo yao, wasije wakageuka nami nikawaponya.”
41
Isaya alisema haya alipoona utukufu wa Yesu na kunena habari zake.
42
Lakini wengi miongoni mwa viongozi wa Wayahudi walimwamini, lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakukiri waziwazi kwa maana waliogopa kufukuzwa katika masinagogi.
43
Wao walipenda sifa za wanadamu kuliko sifa zitokazo kwa Mungu.
Settings