Yohana 1:4-9
4
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
5
Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
6
Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
7
Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
8
Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
9
Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
Settings