Ayubu 7:17-21
17
“Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki, kwamba unamtia sana maanani,
18
kwamba unamwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?
19
Je, hutaacha kamwe kunitazama, au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
20
Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini, Ewe mlinzi wa wanadamu? Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako?
21
Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”
Settings