Skip to content
Ayubu 39:1-8

Ayubu 39:1-8

1
“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
2
Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
3
Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
4
Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
5
“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
6
Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
7
Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
8
Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options