Ayubu 38:39
Inaonyesha mstari 39 pamoja na muktadha unaouzunguka.
36
Ni nani aliyeujalia moyo hekima au kuzipa akili ufahamu?
37
Nani mwenye hekima ya kuyahesabu mawingu? Ni nani awezaye kuinamisha magudulia ya mbinguni
38
wakati mavumbi yawapo magumu, na mabonge ya udongo kushikamana pamoja?
39
“Je, utamwindia simba jike mawindo, na kuwashibisha simba wenye njaa
40
wakati wao wamejikunyata mapangoni mwao, au wakivizia kichakani?
41
Ni nani ampaye kunguru chakula wakati makinda yake yanamlilia Mungu, yakizungukazunguka kwa ajili ya kukosa chakula?
Settings