Ayubu 37:9-13
9
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Settings