Ayubu 37:6-13
6
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
Settings