Skip to content
Ayubu 33:1-7

Ayubu 33:1-7

1
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options