Skip to content
Ayubu 32:15-22

Ayubu 32:15-22

15
“Wametiwa hofu na hawana la zaidi la kusema; maneno yamewaishia.
16
Je, ningoje sasa kwa sababu wamekuwa kimya, kwa vile sasa wanasimama bila kuwa na la kujibu?
17
Mimi nami nitakuwa na la kusema; mimi nami nitasema lile nilijualo.
18
Kwa kuwa nimejawa na maneno, nayo Roho iliyomo ndani yangu yanisukuma;
19
ndani yangu niko kama chupa iliyojazwa divai, kama kiriba kipya cha divai kilicho tayari kupasuka.
20
Ni lazima niseme ili niweze kutulia; ni lazima nifumbue midomo yangu nipate kujibu.
21
Sitampendelea mtu yeyote, wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote;
22
kwa kuwa kama ningekuwa stadi wa kujipendekeza, Muumba wangu angeniondolea mbali kwa upesi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options