Ayubu 29:7-11
7
“Wakati nilipokwenda kwenye lango la mji na kuketi katika kiwanja,
8
vijana waliniona wakakaa kando, nao wazee walioketi wakasimama;
9
wakuu wakaacha kuzungumza na kuziba vinywa vyao kwa mikono yao;
10
wenye vyeo wakanyamazishwa, nazo ndimi zao zikagandamana na makaakaa ya vinywa vyao.
11
Yeyote aliyenisikia alinena mema juu yangu, nao walioniona walinisifu,
Settings