Ayubu 27:5-12
5
Sitakubaliana nanyi kabisa kuwa mko sahihi; hadi nife, sitakana uadilifu wangu.
6
Nitadumisha haki yangu wala sitaiacha; dhamiri yangu haitanisuta muda wote ninaoishi.
7
“Watesi wangu wawe kama waovu, nao adui zangu wawe kama wasio haki!
8
Kwa maana mtu asiyemcha Mungu analo tegemeo gani anapokatiliwa mbali, Mungu anapouondoa uhai wake?
9
Je, Mungu husikiliza kilio chake, shida zimjiapo?
10
Je, anaweza kumfurahia Mwenyezi? Je, atamwita Mungu nyakati zote?
11
“Nitawafundisha juu ya uweza wa Mungu; njia za Mwenyezi sitazificha.
12
Ninyi nyote mmeona hili wenyewe. Ni ya nini basi mazungumzo haya yasiyo na maana?
Settings