Ayubu 23:3-9
3
Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
4
Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
5
Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
6
Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
7
Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
8
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
9
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
Settings