Skip to content
Ayubu 21:7-13

Ayubu 21:7-13

7
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?
8
Huwaona watoto wao wakithibitika wakiwa wamewazunguka, wazao wao mbele za macho yao.
9
Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu; fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10
Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe; ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.
11
Huwatoa watoto wao nje kama kundi; wadogo wao huchezacheza.
12
Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi, nao huifurahia sauti ya filimbi.
13
Huitumia miaka yao katika mafanikio nao hushuka kaburini kwa amani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options