Ayubu 21:7-13
7
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wakifikia umri wa uzee na kuendelea kuwa na nguvu?
8
Huwaona watoto wao wakithibitika wakiwa wamewazunguka, wazao wao mbele za macho yao.
9
Nyumba zao zi salama wala hakuna hofu; fimbo ya Mungu haiko juu yao.
10
Madume yao ya ngʼombe huvyaza bila kushindwa kamwe; ngʼombe wao huzaa wala hawaharibu mimba.
11
Huwatoa watoto wao nje kama kundi; wadogo wao huchezacheza.
12
Huimba nyimbo kwa matari na kwa kinubi, nao huifurahia sauti ya filimbi.
13
Huitumia miaka yao katika mafanikio nao hushuka kaburini kwa amani.
Settings