Skip to content
Ayubu 21:1-6

Ayubu aomba asikilizwe kwa makini

Ayubu 21:1-6
1
Ndipo Ayubu akajibu:
2
“Yasikilizeni maneno yangu kwa makini; hii na iwe faraja mnayonipa mimi.
3
Nivumilieni ninapozungumza, nami nikishazungumza, endeleeni kunidhihaki.
4
“Je, kwani malalamiko yangu yanaelekezwa kwa mwanadamu? Kwa nini nisikose subira?
5
Niangalieni mkastaajabu; mkaweke mkono juu ya vinywa vyenu.
6
Ninapowaza juu ya hili, ninaogopa, nao mwili wangu unatetemeka.
Settings

Reading style

Typeface

Font size 19px

Reading width 90 chars

Options