Ayubu 20:4-9
4
“Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani, tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,
5
macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.
6
Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni na kichwa chake hugusa mawingu,
7
ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe. Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’
8
Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena, amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.
9
Jicho lililomwona halitamwona tena; mahali pake hapatamwona tena.
Settings