Ayubu 18:9
Inaonyesha mstari 9 pamoja na muktadha unaouzunguka.
6
Mwanga hemani mwake umekuwa giza; taa iliyo karibu naye imezimika.
7
Nguvu za hatua zake zimedhoofishwa; shauri lake baya litamwangusha.
8
Miguu yake imemsukumia kwenye wavu, naye anatangatanga kwenye matundu ya wavu.
9
Tanzi litamkamata kwenye kisigino; mtego utamshikilia kwa nguvu.
10
Kitanzi kimefichwa ardhini kwa ajili yake; mtego uko kwenye njia yake.
11
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
Settings