Skip to content
Ayubu 18:11-21

Ayubu 18:11-21

11
Vitisho vimemtia hofu kila upande, na adui zake humwandama kila hatua.
12
Janga linamwonea shauku; maafa yako tayari kwa ajili yake aangukapo.
13
Nayo yatakula sehemu ya ngozi yake; mzaliwa wa kwanza wa mauti atakula maungo yake.
14
Atangʼolewa kutoka usalama wa hema lake, na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15
Moto utakaa katika hema lake; moto wa kiberiti utamwagwa juu ya makao yake.
16
Mizizi yake chini itakauka na matawi yake juu yatanyauka.
17
Kumbukumbu lake litatoweka katika dunia, wala hatakuwa na jina katika nchi.
18
Ameondolewa nuruni na kusukumiwa gizani, naye amefukuzwa mbali atoke duniani.
19
Hana mtoto wala mzao miongoni mwa watu wake, wala aliyenusurika mahali alipoishi.
20
Watu wa magharibi watashangaa yaliyompata; watu wa mashariki watapatwa na hofu.
21
Hakika ndivyo yalivyo makao ya mtu mwovu; ndivyo palivyo mahali pake mtu asiyemjua Mungu.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options