Skip to content
Ayubu 16:9-14

Ayubu 16:9-14

9
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options