Rukia maudhui
Ayubu 13:13-19

Azimio la Ayubu: imani licha ya kifo

Ayubu 13:13-19
13
“Nyamazeni kimya nipate kusema; kisha na yanipate yatakayonipata.
14
Kwa nini nijiweke mwenyewe kwenye hatari na kuyaweka maisha yangu mikononi mwangu?
15
Ingawa ataniua, bado nitamtumaini; hakika nitazitetea njia zangu mbele zake.
16
Naam, hili litanigeukia kuwa wokovu wangu, kwa maana hakuna mtu asiyemcha Mungu atakayethubutu kuja mbele yake!
17
Sikilizeni maneno yangu kwa makini; nayo masikio yenu yaingize kile nisemacho.
18
Sasa kwamba nimekwisha kutayarisha mambo yangu, ninajua mimi nitahesabiwa kuwa na haki.
19
Je, kuna yeyote anayeweza kuleta mashtaka dhidi yangu? Kama ndivyo, nitanyamaza kimya na nife.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options