Ayubu 12:7-9
7
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?