Rukia maudhui
Yakobo 4:11-12

Onyo Dhidi ya Kuwahukumu Wengine

Yakobo 4:11-12
11
Ndugu, msineneane mabaya ninyi kwa ninyi. Mtu yeyote anayesema mabaya dhidi ya ndugu yake au kumhukumu anasema dhidi ya sheria na kuihukumu. Unapoihukumu sheria, basi huishiki sheria bali umekuwa hakimu wa kuihukumu hiyo sheria.
12
Yuko Mtoa sheria mmoja tu na yeye peke yake ndiye Hakimu, ndiye awezaye kuokoa au kuangamiza. Lakini wewe ni nani hata umhukumu jirani yako?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options