Skip to content
Yakobo 1:2-8

Yakobo 1:2-8

2
Ndugu zangu, hesabuni kuwa ni furaha tupu mnapopatwa na majaribu mbalimbali,
3
kwa sababu mnajua ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
4
Saburi na iwe na kazi timilifu, ili mpate kuwa wakamilifu, mmekamilishwa, bila kupungukiwa na kitu chochote.
5
Kama mtu yeyote miongoni mwenu amepungukiwa na hekima na amwombe Mungu, yeye awapaye watu wote kwa ukarimu wala hana kinyongo, naye atapewa.
6
Lakini anapoomba, lazima aamini wala asiwe na shaka, kwa sababu mtu aliye na shaka ni kama wimbi la bahari, lililochukuliwa na upepo na kutupwa huku na huku.
7
Mtu kama huyo asidhani ya kuwa atapata kitu chochote kutoka kwa Bwana.
8
Yeye ni mtu mwenye nia mbili, mwenye kusitasita katika njia zake zote.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options