Yakobo 1:1
Inaonyesha mstari 1 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Yakobo, mtumwa wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo: Kwa makabila kumi na mawili yaliyotawanyika ulimwenguni: Salamu.
2
Ndugu zangu, hesabuni kuwa ni furaha tupu mnapopatwa na majaribu mbalimbali,
3
kwa sababu mnajua ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi.
4
Saburi na iwe na kazi timilifu, ili mpate kuwa wakamilifu, mmekamilishwa, bila kupungukiwa na kitu chochote.
Settings