Hosea 6:7-10
7
Wamevunja Agano kama Adamu: huko hawakuwa waaminifu kwangu.
8
Gileadi ni mji wenye watu waovu, umetiwa madoa kwa nyayo za damu.
9
Kama wanyangʼanyi wamviziavyo mtu, ndivyo magenge ya makuhani wafanyavyo; wanaulia watu kwenye njia iendayo Shekemu, wakifanya uhalifu wa aibu.
10
Nimeona jambo la kutisha katika nyumba ya Israeli. Huko Efraimu amejitolea kwa ukahaba na Israeli amenajisika.
Settings