Hosea 13:4-8
4
“Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewaleta ninyi toka Misri. Msimkubali Mungu mwingine ila mimi, hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.
5
Niliwatunza huko jangwani, katika nchi yenye joto liunguzalo.
6
Nilipowalisha, walishiba, waliposhiba, wakajivuna, kisha wakanisahau mimi.
7
Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba, kama chui nitawavizia kando ya njia.
8
Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, nitawashambulia na kurarua vifua vyenu. Kama simba nitawala; mnyama pori atawararua vipande vipande.
Settings