Rukia maudhui
Mwanzo 6:9-13

Mwanzo 6:9-13

9
Hivi ndivyo vizazi vya Noa. Noa alikuwa mtu wa haki, na mkamilifu miongoni mwa watu wa wakati wake, tena alitembea na Mungu.
10
Noa alikuwa na wana watatu: Shemu, Hamu na Yafethi.
11
Wakati huu dunia ilikuwa imejaa uharibifu na ukatili machoni pa Mungu.
12
Mungu akaona jinsi dunia ilivyoharibika, kwa maana watu wote duniani walikuwa wameharibu njia zao.
13
Kwa hiyo Mungu akamwambia Noa, “Nitawaangamiza watu wote, kwa kuwa dunia imejaa ukatili kwa sababu yao. Hakika mimi nitaangamiza watu pamoja na dunia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options