Rukia maudhui
Mwanzo 38:27-30

Kuzaliwa kwa Peresi na Zera

Mwanzo 38:27-30
27
Wakati ulipofika wa kujifungua, kukawa na wana mapacha tumboni mwake.
28
Alipokuwa akijifungua, mmoja akatoa mkono wake nje, kwa hiyo mkunga akachukua uzi mwekundu na kuufunga mkononi mwa yule mtoto, akasema, “Huyu ametoka kwanza.”
29
Lakini alipourudisha mkono wake ndugu yake akaanza kutoka, naye akasema, “Hivi ndivyo ulivyotoka kwa nguvu!” Akaitwa Peresi.
30
Kisha ndugu yake, aliyekuwa na uzi mwekundu mkononi, akatoka, naye akaitwa Zera.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options