Rukia maudhui
Kumbukumbu 32:7-10

Kumbukumbu 32:7-10

7
Kumbuka siku za kale; tafakari vizazi vya zamani vilivyopita. Uliza baba yako, naye atakuambia, wazee wako, nao watakueleza.
8
Aliye Juu Sana alipowapa mataifa urithi wao, alipogawanya wanadamu wote, aliweka mipaka kwa ajili ya mataifa sawasawa na hesabu ya wana wa Israeli.
9
Kwa kuwa fungu la Bwana ni watu wake, Yakobo kura yake ya urithi.
10
Katika nchi ya jangwa alimkuta, katika nyika tupu ivumayo upepo. Alimhifadhi na kumtunza; akamlinda kama mboni ya jicho lake,
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options