Rukia maudhui
Kumbukumbu 11:26-32

Chaguo Lililowekwa Mbele ya Israeli

Kumbukumbu 11:26-32
26
Tazama, leo ninaweka mbele yenu baraka na laana:
27
baraka kama mtatii maagizo ya Bwana Mungu wenu, ambayo ninawapa leo;
28
laana kama hamtatii maagizo ya Bwana Mungu wenu na kuacha njia ambayo ninawaamuru leo kwa kufuata miungu mingine, ambayo hamkuijua.
29
Wakati Bwana Mungu wenu atakapokuwa amewaleta katika nchi mnayoiingia kuimiliki, mtatangaza baraka kutoka Mlima Gerizimu, na kutangaza laana kutoka Mlima Ebali.
30
Kama mnavyofahamu, milima hii ipo ngʼambo ya Yordani, magharibi ya barabara, kuelekea machweo ya jua, karibu na miti mikubwa ya More, katika nchi ya wale Wakanaani wanaoishi Araba, jirani na Gilgali.
31
Karibu mvuke ngʼambo ya Yordani kuingia na kuimiliki nchi ambayo Bwana Mungu wenu anawapa. Wakati mtakapokuwa mmeichukua na mnaishi humo,
32
hakikisheni kwamba mnatii amri na sheria zote ninazoziweka mbele yenu leo.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options